Mit. 14:1-11 Swahili Union Version (SUV)

1. Kila mwanamke aliye na hekima hujenga nyumba yake;Bali aliye mpumbavu huibomoa kwa mikono yake mwenyewe.

2. Yeye aendaye kwa unyofu wake humcha BWANA;Bali aliye mkaidi katika njia zake humdharau.

3. Katika kinywa cha mpumbavu mna fimbo ya kiburi,Bali midomo ya wenye hekima huwahifadhi.

4. Zizi ni safi ambapo hapana ng’ombe;Bali nguvu za ng’ombe zaleta faida nyingi.

5. Shahidi mwaminifu hatasema uongo;Bali shahidi wa uongo, pumzi zake ni uongo.

6. Mwenye dharau hutafuta hekima, asiipate;Bali maarifa huwa mepesi kwa mwenye ufahamu.

7. Toka mbele ya uso wa mpumbavu,Maana hutaona kwake midomo ya maarifa.

8. Akili za mwenye busara ni kujua njia yake;Lakini upumbavu wa wapumbavu ni udanganyifu.

9. Wapumbavu huidharau hatia;Bali upo upendeleo kwa wenye haki.

10. Moyo huujua uchungu wa nafsi yake,Wala mgeni haishiriki furaha yake.

11. Nyumba ya mtu mbaya itabomolewa;Bali hema ya mwenye haki itafanikiwa.

Mit. 14