6. Haki humlinda yeye aliye mnyofu katika njia yake;Bali ubaya humwangusha mwenye dhambi.
7. Kuna mtu mwenye kujitajirisha, lakini hana kitu;Kuna ajifanyaye kuwa maskini, lakini ana mali nyingi.
8. Dia ya nafsi ya mtu ni utajiri wake;Bali mtu maskini hasikii ogofyo lo lote.
9. Nuru ya mwenye haki yang’aa sana;Bali taa ya mtu mbaya itazimika.
10. Kiburi huleta mashindano tu;Bali hekima hukaa nao wanaoshauriana.
11. Mali iliyopatikana kwa haraka itapunguka;Bali yeye achumaye kidogo kidogo atazidishiwa.
12. Kilichotarajiwa kikikawia kuja, moyo huugua.Bali haja ya mtu ikipatikana, ni mti wa uzima.