17. Mjumbe mbaya huanguka maovuni;Bali mjumbe mwaminifu ni afya.
18. Umaskini na fedheha zitampata yeye akataaye kurudiwa;Bali yeye aangaliaye maonyo ataheshimiwa.
19. Haja iliyopatikana ni tamu nafsini mwa mtu;Bali kujitenga na maovu ni chukizo kwa wapumbavu.
20. Enenda pamoja na wenye hekima, nawe utakuwa na hekima;Bali rafiki wa wapumbavu ataumia.
21. Uovu huwaandamia wenye dhambi;Bali mwenye haki atalipwa mema.