Mit. 13:17-21 Swahili Union Version (SUV)

17. Mjumbe mbaya huanguka maovuni;Bali mjumbe mwaminifu ni afya.

18. Umaskini na fedheha zitampata yeye akataaye kurudiwa;Bali yeye aangaliaye maonyo ataheshimiwa.

19. Haja iliyopatikana ni tamu nafsini mwa mtu;Bali kujitenga na maovu ni chukizo kwa wapumbavu.

20. Enenda pamoja na wenye hekima, nawe utakuwa na hekima;Bali rafiki wa wapumbavu ataumia.

21. Uovu huwaandamia wenye dhambi;Bali mwenye haki atalipwa mema.

Mit. 13