Mit. 13:14-19 Swahili Union Version (SUV)

14. Sheria ya mwenye akili ni chemchemi ya uzima,Ili kuepukana na tanzi za mauti.

15. Ufahamu mwema huleta upendeleo;Bali njia ya haini huparuza.

16. Kila aliye na busara hutenda kazi kwa maarifa;Bali mpumbavu hueneza upumbavu.

17. Mjumbe mbaya huanguka maovuni;Bali mjumbe mwaminifu ni afya.

18. Umaskini na fedheha zitampata yeye akataaye kurudiwa;Bali yeye aangaliaye maonyo ataheshimiwa.

19. Haja iliyopatikana ni tamu nafsini mwa mtu;Bali kujitenga na maovu ni chukizo kwa wapumbavu.

Mit. 13