5. Mawazo ya mwenye haki ni adili;Bali mashauri ya mtu mwovu ni hadaa.
6. Maneno ya waovu huotea damu;Bali kinywa cha wanyofu kitawaokoa.
7. Waovu huangamia, hata hawako tena;Bali nyumba ya mwenye haki itasimama.
8. Mtu atasifiwa kwa kadiri ya akili zake;Bali mwenye moyo wa ukaidi atadharauliwa.
9. Afadhali mtu anayedharauliwa, ikiwa ana mtumwa,Kuliko ajisifuye, ikiwa anahitaji chakula.
10. Mwenye haki huufikiri uhai wa mnyama wake;Bali huruma za mtu mwovu ni ukatili.
11. Alimaye shamba lake atakuwa na chakula tele;Bali afuataye mambo ya upuzi hana ufahamu.
12. Asiye haki hutamani nyavu za wabaya;Bali shina lao wenye haki huleta matunda.
13. Katika kosa la midomo kuna mtego kwa mbaya;Bali mwenye haki atatoka katika taabu.
14. Mtu atashiba mema kwa matunda ya kinywa chake;Na atarudishiwa matendo ya mikono yake.
15. Njia ya mpumbavu imenyoka machoni pake mwenyewe;Bali yeye aliye na hekima husikiliza shauri.
16. Ghadhabu ya mpumbavu hujulika mara;Bali mtu mwerevu husitiri aibu.
17. Atamkaye maneno ya kweli hufunua haki;Bali shahidi wa uongo hutamka hila.
18. Kuna anenaye bila kufikiri, kama kuchoma kwa upanga;Bali ulimi wa mwenye haki ni afya.
19. Mdomo wa kweli utathibitishwa milele;Bali ulimi wa uongo ni wa kitambo tu.