4. Mwanamke mwema ni taji ya mumewe;Bali aaibishaye ni kama kuoza mifupani mwake.
5. Mawazo ya mwenye haki ni adili;Bali mashauri ya mtu mwovu ni hadaa.
6. Maneno ya waovu huotea damu;Bali kinywa cha wanyofu kitawaokoa.
7. Waovu huangamia, hata hawako tena;Bali nyumba ya mwenye haki itasimama.
8. Mtu atasifiwa kwa kadiri ya akili zake;Bali mwenye moyo wa ukaidi atadharauliwa.
9. Afadhali mtu anayedharauliwa, ikiwa ana mtumwa,Kuliko ajisifuye, ikiwa anahitaji chakula.
10. Mwenye haki huufikiri uhai wa mnyama wake;Bali huruma za mtu mwovu ni ukatili.
11. Alimaye shamba lake atakuwa na chakula tele;Bali afuataye mambo ya upuzi hana ufahamu.
12. Asiye haki hutamani nyavu za wabaya;Bali shina lao wenye haki huleta matunda.
13. Katika kosa la midomo kuna mtego kwa mbaya;Bali mwenye haki atatoka katika taabu.