Mit. 12:4-11 Swahili Union Version (SUV)

4. Mwanamke mwema ni taji ya mumewe;Bali aaibishaye ni kama kuoza mifupani mwake.

5. Mawazo ya mwenye haki ni adili;Bali mashauri ya mtu mwovu ni hadaa.

6. Maneno ya waovu huotea damu;Bali kinywa cha wanyofu kitawaokoa.

7. Waovu huangamia, hata hawako tena;Bali nyumba ya mwenye haki itasimama.

8. Mtu atasifiwa kwa kadiri ya akili zake;Bali mwenye moyo wa ukaidi atadharauliwa.

9. Afadhali mtu anayedharauliwa, ikiwa ana mtumwa,Kuliko ajisifuye, ikiwa anahitaji chakula.

10. Mwenye haki huufikiri uhai wa mnyama wake;Bali huruma za mtu mwovu ni ukatili.

11. Alimaye shamba lake atakuwa na chakula tele;Bali afuataye mambo ya upuzi hana ufahamu.

Mit. 12