Mit. 12:24-27 Swahili Union Version (SUV)

24. Mkono wa mwenye bidii utatawala;Bali mvivu atalipishwa kodi.

25. Uzito katika moyo wa mtu huuinamisha;Bali neno jema huufurahisha.

26. Mwenye haki ni kiongozi cha mwenzake;Bali njia ya wasio haki huwakosesha.

27. Mtu mvivu hapiki mawindo yake;Bali mwenye bidii anazo mali za thamani.

Mit. 12