20. Hila imo mioyoni mwao wafikirio uovu;Bali wafanyao mashauri ya amani, kwao kuna furaha.
21. Mwenye haki hatapatikana na msiba wo wote;Bali wasio haki watajazwa mabaya.
22. Midomo ya uongo ni chukizo kwa BWANA;Bali watendao uaminifu ndio furaha yake.
23. Mwanadamu mwenye busara husitiri maarifa;Bali moyo wa wapumbavu hutangaza upumbavu.
24. Mkono wa mwenye bidii utatawala;Bali mvivu atalipishwa kodi.
25. Uzito katika moyo wa mtu huuinamisha;Bali neno jema huufurahisha.
26. Mwenye haki ni kiongozi cha mwenzake;Bali njia ya wasio haki huwakosesha.
27. Mtu mvivu hapiki mawindo yake;Bali mwenye bidii anazo mali za thamani.