18. Kuna anenaye bila kufikiri, kama kuchoma kwa upanga;Bali ulimi wa mwenye haki ni afya.
19. Mdomo wa kweli utathibitishwa milele;Bali ulimi wa uongo ni wa kitambo tu.
20. Hila imo mioyoni mwao wafikirio uovu;Bali wafanyao mashauri ya amani, kwao kuna furaha.
21. Mwenye haki hatapatikana na msiba wo wote;Bali wasio haki watajazwa mabaya.
22. Midomo ya uongo ni chukizo kwa BWANA;Bali watendao uaminifu ndio furaha yake.
23. Mwanadamu mwenye busara husitiri maarifa;Bali moyo wa wapumbavu hutangaza upumbavu.