Mit. 12:14-19 Swahili Union Version (SUV)

14. Mtu atashiba mema kwa matunda ya kinywa chake;Na atarudishiwa matendo ya mikono yake.

15. Njia ya mpumbavu imenyoka machoni pake mwenyewe;Bali yeye aliye na hekima husikiliza shauri.

16. Ghadhabu ya mpumbavu hujulika mara;Bali mtu mwerevu husitiri aibu.

17. Atamkaye maneno ya kweli hufunua haki;Bali shahidi wa uongo hutamka hila.

18. Kuna anenaye bila kufikiri, kama kuchoma kwa upanga;Bali ulimi wa mwenye haki ni afya.

19. Mdomo wa kweli utathibitishwa milele;Bali ulimi wa uongo ni wa kitambo tu.

Mit. 12