12. Asiye haki hutamani nyavu za wabaya;Bali shina lao wenye haki huleta matunda.
13. Katika kosa la midomo kuna mtego kwa mbaya;Bali mwenye haki atatoka katika taabu.
14. Mtu atashiba mema kwa matunda ya kinywa chake;Na atarudishiwa matendo ya mikono yake.
15. Njia ya mpumbavu imenyoka machoni pake mwenyewe;Bali yeye aliye na hekima husikiliza shauri.
16. Ghadhabu ya mpumbavu hujulika mara;Bali mtu mwerevu husitiri aibu.
17. Atamkaye maneno ya kweli hufunua haki;Bali shahidi wa uongo hutamka hila.
18. Kuna anenaye bila kufikiri, kama kuchoma kwa upanga;Bali ulimi wa mwenye haki ni afya.
19. Mdomo wa kweli utathibitishwa milele;Bali ulimi wa uongo ni wa kitambo tu.
20. Hila imo mioyoni mwao wafikirio uovu;Bali wafanyao mashauri ya amani, kwao kuna furaha.
21. Mwenye haki hatapatikana na msiba wo wote;Bali wasio haki watajazwa mabaya.