1. Kila apendaye mafundisho hupenda maarifa;Bali yeye achukiaye kulaumiwa ni kama mnyama.
2. Mtu mwema atapata upendeleo kwa BWANA;Bali mtu wa hila atahukumiwa naye.
3. Mtu hatathibitika kwa njia ya uovu;Shina la mwenye haki halitaondolewa kamwe.
4. Mwanamke mwema ni taji ya mumewe;Bali aaibishaye ni kama kuoza mifupani mwake.
5. Mawazo ya mwenye haki ni adili;Bali mashauri ya mtu mwovu ni hadaa.
6. Maneno ya waovu huotea damu;Bali kinywa cha wanyofu kitawaokoa.
7. Waovu huangamia, hata hawako tena;Bali nyumba ya mwenye haki itasimama.
8. Mtu atasifiwa kwa kadiri ya akili zake;Bali mwenye moyo wa ukaidi atadharauliwa.
9. Afadhali mtu anayedharauliwa, ikiwa ana mtumwa,Kuliko ajisifuye, ikiwa anahitaji chakula.