Mit. 12:1-13 Swahili Union Version (SUV)

1. Kila apendaye mafundisho hupenda maarifa;Bali yeye achukiaye kulaumiwa ni kama mnyama.

2. Mtu mwema atapata upendeleo kwa BWANA;Bali mtu wa hila atahukumiwa naye.

3. Mtu hatathibitika kwa njia ya uovu;Shina la mwenye haki halitaondolewa kamwe.

4. Mwanamke mwema ni taji ya mumewe;Bali aaibishaye ni kama kuoza mifupani mwake.

5. Mawazo ya mwenye haki ni adili;Bali mashauri ya mtu mwovu ni hadaa.

6. Maneno ya waovu huotea damu;Bali kinywa cha wanyofu kitawaokoa.

7. Waovu huangamia, hata hawako tena;Bali nyumba ya mwenye haki itasimama.

8. Mtu atasifiwa kwa kadiri ya akili zake;Bali mwenye moyo wa ukaidi atadharauliwa.

9. Afadhali mtu anayedharauliwa, ikiwa ana mtumwa,Kuliko ajisifuye, ikiwa anahitaji chakula.

10. Mwenye haki huufikiri uhai wa mnyama wake;Bali huruma za mtu mwovu ni ukatili.

11. Alimaye shamba lake atakuwa na chakula tele;Bali afuataye mambo ya upuzi hana ufahamu.

12. Asiye haki hutamani nyavu za wabaya;Bali shina lao wenye haki huleta matunda.

13. Katika kosa la midomo kuna mtego kwa mbaya;Bali mwenye haki atatoka katika taabu.

Mit. 12