9. Asiyemcha Mungu humpoteza jirani yake kwa kinywa chake;Bali wenye haki watapona kwa maarifa.
10. Wenye haki wasitawipo, mji hufurahi;Waovu waangamiapo, watu hupiga kelele.
11. Mji hutukuzwa kwa mbaraka wa mwenye haki;Bali mji hupinduliwa kwa kinywa cha mwovu.
12. Asiye na akili humdharau mwenziwe;Bali mtu aliye na ufahamu hunyamaza.
13. Mwenye kitango akisingizia hufunua siri;Bali mwenye roho ya uaminifu husitiri mambo.
14. Pasipo mashauri taifa huanguka;Bali kwa wingi wa washauri huja wokovu.
15. Amdhaminiye mgeni hakosi ataumia;Achukiaye mambo ya dhamana yu salama.
16. Mwanamke wa adabu huheshimiwa daima;Na watu wakali hushika mali siku zote.
17. Mwenye rehema huitendea mema nafsi yake;Aliye mkali hujisumbua mwili wake.
18. Mtu mwovu hupata mshahara wa udanganyifu;Apandaye haki ana thawabu ya hakika.
19. Haki huelekea uzima;Afuataye maovu hufuata mauti yake mwenyewe.
20. Wenye kuhalifu moyoni ni chukizo kwa BWANA;Walio wakamilifu katika njia zao humpendeza.
21. Hakika, mtu mwovu hatakosa adhabu;Bali wazao wa wenye haki wataokoka.
22. Kama pete ya dhahabu katika pua ya nguruwe,Kadhalika mwanamke mzuri asiye na akili.
23. Haja ya mwenye haki ni mema tu;Bali kutaraji kwake mtu mwovu ni ghadhabu.
24. Kuna atawanyaye, lakini huongezewa zaidi;Kuna azuiaye isivyo haki, lakini huelekea uhitaji.
25. Nafsi ya mtu mkarimu itawandishwa;Anyweshaye atanyweshwa mwenyewe.
26. Awanyimaye watu nafaka, watu watamlaani;Auzaye nafaka, baraka itakuwa kichwani pake.