Mit. 11:6-8 Swahili Union Version (SUV)

6. Haki yao wenye haki itawaokoa;Bali wafanyao fitina watanaswa kwa hila yao wenyewe.

7. Mtu mwovu atakapokufa, taraja lake lapotea;Na matumaini ya uovu huangamia.

8. Mwenye haki huokolewa katika dhiki,Na mtu mwovu ataiingia badala yake.

Mit. 11