6. Haki yao wenye haki itawaokoa;Bali wafanyao fitina watanaswa kwa hila yao wenyewe.
7. Mtu mwovu atakapokufa, taraja lake lapotea;Na matumaini ya uovu huangamia.
8. Mwenye haki huokolewa katika dhiki,Na mtu mwovu ataiingia badala yake.
9. Asiyemcha Mungu humpoteza jirani yake kwa kinywa chake;Bali wenye haki watapona kwa maarifa.
10. Wenye haki wasitawipo, mji hufurahi;Waovu waangamiapo, watu hupiga kelele.
11. Mji hutukuzwa kwa mbaraka wa mwenye haki;Bali mji hupinduliwa kwa kinywa cha mwovu.
12. Asiye na akili humdharau mwenziwe;Bali mtu aliye na ufahamu hunyamaza.
13. Mwenye kitango akisingizia hufunua siri;Bali mwenye roho ya uaminifu husitiri mambo.