Mit. 11:6-13 Swahili Union Version (SUV)

6. Haki yao wenye haki itawaokoa;Bali wafanyao fitina watanaswa kwa hila yao wenyewe.

7. Mtu mwovu atakapokufa, taraja lake lapotea;Na matumaini ya uovu huangamia.

8. Mwenye haki huokolewa katika dhiki,Na mtu mwovu ataiingia badala yake.

9. Asiyemcha Mungu humpoteza jirani yake kwa kinywa chake;Bali wenye haki watapona kwa maarifa.

10. Wenye haki wasitawipo, mji hufurahi;Waovu waangamiapo, watu hupiga kelele.

11. Mji hutukuzwa kwa mbaraka wa mwenye haki;Bali mji hupinduliwa kwa kinywa cha mwovu.

12. Asiye na akili humdharau mwenziwe;Bali mtu aliye na ufahamu hunyamaza.

13. Mwenye kitango akisingizia hufunua siri;Bali mwenye roho ya uaminifu husitiri mambo.

Mit. 11