4. Mali hazifaidii kitu siku ya ghadhabu;Bali haki huokoa na mauti.
5. Haki yake mtu mkamilifu itamwongoza njia yake;Bali mtu mwovu ataanguka kwa uovu wake.
6. Haki yao wenye haki itawaokoa;Bali wafanyao fitina watanaswa kwa hila yao wenyewe.
7. Mtu mwovu atakapokufa, taraja lake lapotea;Na matumaini ya uovu huangamia.
8. Mwenye haki huokolewa katika dhiki,Na mtu mwovu ataiingia badala yake.
9. Asiyemcha Mungu humpoteza jirani yake kwa kinywa chake;Bali wenye haki watapona kwa maarifa.
10. Wenye haki wasitawipo, mji hufurahi;Waovu waangamiapo, watu hupiga kelele.
11. Mji hutukuzwa kwa mbaraka wa mwenye haki;Bali mji hupinduliwa kwa kinywa cha mwovu.
12. Asiye na akili humdharau mwenziwe;Bali mtu aliye na ufahamu hunyamaza.
13. Mwenye kitango akisingizia hufunua siri;Bali mwenye roho ya uaminifu husitiri mambo.
14. Pasipo mashauri taifa huanguka;Bali kwa wingi wa washauri huja wokovu.
15. Amdhaminiye mgeni hakosi ataumia;Achukiaye mambo ya dhamana yu salama.
16. Mwanamke wa adabu huheshimiwa daima;Na watu wakali hushika mali siku zote.
17. Mwenye rehema huitendea mema nafsi yake;Aliye mkali hujisumbua mwili wake.