26. Awanyimaye watu nafaka, watu watamlaani;Auzaye nafaka, baraka itakuwa kichwani pake.
27. Atafutaye mema kwa bidii hutafuta fadhili;Atafutaye madhara, hayo yatamjia.
28. Azitegemeaye mali zake ataanguka;Mwenye haki atasitawi kama jani.
29. Ataabishaye nyumba yake mwenyewe ataurithi upepo;Mpumbavu atakuwa mtumwa wa mtu mwenye moyo wa akili.
30. Mazao ya mwenye haki ni mti wa uzima;Na mwenye hekima huvuta roho za watu.