22. Kama pete ya dhahabu katika pua ya nguruwe,Kadhalika mwanamke mzuri asiye na akili.
23. Haja ya mwenye haki ni mema tu;Bali kutaraji kwake mtu mwovu ni ghadhabu.
24. Kuna atawanyaye, lakini huongezewa zaidi;Kuna azuiaye isivyo haki, lakini huelekea uhitaji.
25. Nafsi ya mtu mkarimu itawandishwa;Anyweshaye atanyweshwa mwenyewe.
26. Awanyimaye watu nafaka, watu watamlaani;Auzaye nafaka, baraka itakuwa kichwani pake.
27. Atafutaye mema kwa bidii hutafuta fadhili;Atafutaye madhara, hayo yatamjia.
28. Azitegemeaye mali zake ataanguka;Mwenye haki atasitawi kama jani.
29. Ataabishaye nyumba yake mwenyewe ataurithi upepo;Mpumbavu atakuwa mtumwa wa mtu mwenye moyo wa akili.
30. Mazao ya mwenye haki ni mti wa uzima;Na mwenye hekima huvuta roho za watu.