Mit. 11:22-30 Swahili Union Version (SUV)

22. Kama pete ya dhahabu katika pua ya nguruwe,Kadhalika mwanamke mzuri asiye na akili.

23. Haja ya mwenye haki ni mema tu;Bali kutaraji kwake mtu mwovu ni ghadhabu.

24. Kuna atawanyaye, lakini huongezewa zaidi;Kuna azuiaye isivyo haki, lakini huelekea uhitaji.

25. Nafsi ya mtu mkarimu itawandishwa;Anyweshaye atanyweshwa mwenyewe.

26. Awanyimaye watu nafaka, watu watamlaani;Auzaye nafaka, baraka itakuwa kichwani pake.

27. Atafutaye mema kwa bidii hutafuta fadhili;Atafutaye madhara, hayo yatamjia.

28. Azitegemeaye mali zake ataanguka;Mwenye haki atasitawi kama jani.

29. Ataabishaye nyumba yake mwenyewe ataurithi upepo;Mpumbavu atakuwa mtumwa wa mtu mwenye moyo wa akili.

30. Mazao ya mwenye haki ni mti wa uzima;Na mwenye hekima huvuta roho za watu.

Mit. 11