Mit. 11:20-23 Swahili Union Version (SUV)

20. Wenye kuhalifu moyoni ni chukizo kwa BWANA;Walio wakamilifu katika njia zao humpendeza.

21. Hakika, mtu mwovu hatakosa adhabu;Bali wazao wa wenye haki wataokoka.

22. Kama pete ya dhahabu katika pua ya nguruwe,Kadhalika mwanamke mzuri asiye na akili.

23. Haja ya mwenye haki ni mema tu;Bali kutaraji kwake mtu mwovu ni ghadhabu.

Mit. 11