Mit. 11:15-26 Swahili Union Version (SUV)

15. Amdhaminiye mgeni hakosi ataumia;Achukiaye mambo ya dhamana yu salama.

16. Mwanamke wa adabu huheshimiwa daima;Na watu wakali hushika mali siku zote.

17. Mwenye rehema huitendea mema nafsi yake;Aliye mkali hujisumbua mwili wake.

18. Mtu mwovu hupata mshahara wa udanganyifu;Apandaye haki ana thawabu ya hakika.

19. Haki huelekea uzima;Afuataye maovu hufuata mauti yake mwenyewe.

20. Wenye kuhalifu moyoni ni chukizo kwa BWANA;Walio wakamilifu katika njia zao humpendeza.

21. Hakika, mtu mwovu hatakosa adhabu;Bali wazao wa wenye haki wataokoka.

22. Kama pete ya dhahabu katika pua ya nguruwe,Kadhalika mwanamke mzuri asiye na akili.

23. Haja ya mwenye haki ni mema tu;Bali kutaraji kwake mtu mwovu ni ghadhabu.

24. Kuna atawanyaye, lakini huongezewa zaidi;Kuna azuiaye isivyo haki, lakini huelekea uhitaji.

25. Nafsi ya mtu mkarimu itawandishwa;Anyweshaye atanyweshwa mwenyewe.

26. Awanyimaye watu nafaka, watu watamlaani;Auzaye nafaka, baraka itakuwa kichwani pake.

Mit. 11