15. Amdhaminiye mgeni hakosi ataumia;Achukiaye mambo ya dhamana yu salama.
16. Mwanamke wa adabu huheshimiwa daima;Na watu wakali hushika mali siku zote.
17. Mwenye rehema huitendea mema nafsi yake;Aliye mkali hujisumbua mwili wake.
18. Mtu mwovu hupata mshahara wa udanganyifu;Apandaye haki ana thawabu ya hakika.
19. Haki huelekea uzima;Afuataye maovu hufuata mauti yake mwenyewe.
20. Wenye kuhalifu moyoni ni chukizo kwa BWANA;Walio wakamilifu katika njia zao humpendeza.
21. Hakika, mtu mwovu hatakosa adhabu;Bali wazao wa wenye haki wataokoka.
22. Kama pete ya dhahabu katika pua ya nguruwe,Kadhalika mwanamke mzuri asiye na akili.
23. Haja ya mwenye haki ni mema tu;Bali kutaraji kwake mtu mwovu ni ghadhabu.
24. Kuna atawanyaye, lakini huongezewa zaidi;Kuna azuiaye isivyo haki, lakini huelekea uhitaji.
25. Nafsi ya mtu mkarimu itawandishwa;Anyweshaye atanyweshwa mwenyewe.
26. Awanyimaye watu nafaka, watu watamlaani;Auzaye nafaka, baraka itakuwa kichwani pake.