13. Mwenye kitango akisingizia hufunua siri;Bali mwenye roho ya uaminifu husitiri mambo.
14. Pasipo mashauri taifa huanguka;Bali kwa wingi wa washauri huja wokovu.
15. Amdhaminiye mgeni hakosi ataumia;Achukiaye mambo ya dhamana yu salama.
16. Mwanamke wa adabu huheshimiwa daima;Na watu wakali hushika mali siku zote.
17. Mwenye rehema huitendea mema nafsi yake;Aliye mkali hujisumbua mwili wake.
18. Mtu mwovu hupata mshahara wa udanganyifu;Apandaye haki ana thawabu ya hakika.