10. Wenye haki wasitawipo, mji hufurahi;Waovu waangamiapo, watu hupiga kelele.
11. Mji hutukuzwa kwa mbaraka wa mwenye haki;Bali mji hupinduliwa kwa kinywa cha mwovu.
12. Asiye na akili humdharau mwenziwe;Bali mtu aliye na ufahamu hunyamaza.
13. Mwenye kitango akisingizia hufunua siri;Bali mwenye roho ya uaminifu husitiri mambo.
14. Pasipo mashauri taifa huanguka;Bali kwa wingi wa washauri huja wokovu.