Mit. 11:10-14 Swahili Union Version (SUV)

10. Wenye haki wasitawipo, mji hufurahi;Waovu waangamiapo, watu hupiga kelele.

11. Mji hutukuzwa kwa mbaraka wa mwenye haki;Bali mji hupinduliwa kwa kinywa cha mwovu.

12. Asiye na akili humdharau mwenziwe;Bali mtu aliye na ufahamu hunyamaza.

13. Mwenye kitango akisingizia hufunua siri;Bali mwenye roho ya uaminifu husitiri mambo.

14. Pasipo mashauri taifa huanguka;Bali kwa wingi wa washauri huja wokovu.

Mit. 11