1. Mizani ya hadaa ni chukizo kwa BWANA;Bali vipimo vilivyo sawasawa humpendeza.
2. Kijapo kiburi ndipo ijapo aibu;Bali hekima hukaa na wanyenyekevu.
3. Ukamilifu wao wenye haki utawaongozaBali ukaidi wao wenye fitina utawaangamiza.
4. Mali hazifaidii kitu siku ya ghadhabu;Bali haki huokoa na mauti.
5. Haki yake mtu mkamilifu itamwongoza njia yake;Bali mtu mwovu ataanguka kwa uovu wake.
6. Haki yao wenye haki itawaokoa;Bali wafanyao fitina watanaswa kwa hila yao wenyewe.
7. Mtu mwovu atakapokufa, taraja lake lapotea;Na matumaini ya uovu huangamia.
8. Mwenye haki huokolewa katika dhiki,Na mtu mwovu ataiingia badala yake.