Mit. 11:1-6 Swahili Union Version (SUV)

1. Mizani ya hadaa ni chukizo kwa BWANA;Bali vipimo vilivyo sawasawa humpendeza.

2. Kijapo kiburi ndipo ijapo aibu;Bali hekima hukaa na wanyenyekevu.

3. Ukamilifu wao wenye haki utawaongozaBali ukaidi wao wenye fitina utawaangamiza.

4. Mali hazifaidii kitu siku ya ghadhabu;Bali haki huokoa na mauti.

5. Haki yake mtu mkamilifu itamwongoza njia yake;Bali mtu mwovu ataanguka kwa uovu wake.

6. Haki yao wenye haki itawaokoa;Bali wafanyao fitina watanaswa kwa hila yao wenyewe.

Mit. 11