1. Mizani ya hadaa ni chukizo kwa BWANA;Bali vipimo vilivyo sawasawa humpendeza.
2. Kijapo kiburi ndipo ijapo aibu;Bali hekima hukaa na wanyenyekevu.
3. Ukamilifu wao wenye haki utawaongozaBali ukaidi wao wenye fitina utawaangamiza.
4. Mali hazifaidii kitu siku ya ghadhabu;Bali haki huokoa na mauti.