Mit. 11:1-4 Swahili Union Version (SUV)

1. Mizani ya hadaa ni chukizo kwa BWANA;Bali vipimo vilivyo sawasawa humpendeza.

2. Kijapo kiburi ndipo ijapo aibu;Bali hekima hukaa na wanyenyekevu.

3. Ukamilifu wao wenye haki utawaongozaBali ukaidi wao wenye fitina utawaangamiza.

4. Mali hazifaidii kitu siku ya ghadhabu;Bali haki huokoa na mauti.

Mit. 11