Mit. 10:8-23 Swahili Union Version (SUV)

8. Aliye na akili moyoni mwake atapokea agizo;Bali mpumbavu mwenye maneno mengi ataanguka.

9. Aendaye kwa unyofu huenda salama;Bali apotoshaye njia zake atajulikana.

10. Akonyezaye kwa jicho huleta masikitiko;Bali mpumbavu mwenye maneno mengi ataanguka.

11. Kinywa chake mwenye haki ni chemchemi ya uzima;Bali jeuri hufunika kinywa chake mtu mwovu,

12. Kuchukiana huondokesha fitina;Bali kupendana husitiri makosa yote.

13. Hekima hupatikana midomoni mwa mwenye ufahamu;Bali fimbo hufaa kwa mgongo wake asiye na ufahamu.

14. Watu wenye akili huweka akiba ya maarifa;Bali kinywa cha mpumbavu ni uangamivu ulio karibu.

15. Mali ya mtu tajiri ni mji wake wa nguvu;Uangamivu wa maskini ni umaskini wao.

16. Kazi yake mwenye haki huuelekea uzima;Mazao ya wabaya huuelekea dhambi.

17. Akubaliye kurudiwa huwa katika njia ya uzima;Bali yeye aachaye maonyo hukosa.

18. Yeye afichaye chuki ana midomo ya uongo,Na yeye asingiziaye ni mpumbavu.

19. Katika wingi wa maneno hapakosi kuwa na maovu;Bali yeye azuiaye midomo yake hufanya akili.

20. Ulimi wa mwenye haki ni kama fedha teule;Moyo wa mtu mbaya haufai kitu.

21. Midomo ya mwenye haki hulisha watu wengi;Bali wapumbavu hufa kwa kuwa hawana ufahamu.

22. Baraka ya BWANA hutajirisha,Wala hachanganyi huzuni nayo.

23. Kwa mpumbavu kutenda maovu ni kama mchezo;Bali mtu mwenye ufahamu ana hekima.

Mit. 10