7. Kuwakumbuka wenye haki huwa na baraka;Bali jina la mtu mwovu litaoza.
8. Aliye na akili moyoni mwake atapokea agizo;Bali mpumbavu mwenye maneno mengi ataanguka.
9. Aendaye kwa unyofu huenda salama;Bali apotoshaye njia zake atajulikana.
10. Akonyezaye kwa jicho huleta masikitiko;Bali mpumbavu mwenye maneno mengi ataanguka.
11. Kinywa chake mwenye haki ni chemchemi ya uzima;Bali jeuri hufunika kinywa chake mtu mwovu,
12. Kuchukiana huondokesha fitina;Bali kupendana husitiri makosa yote.
13. Hekima hupatikana midomoni mwa mwenye ufahamu;Bali fimbo hufaa kwa mgongo wake asiye na ufahamu.
14. Watu wenye akili huweka akiba ya maarifa;Bali kinywa cha mpumbavu ni uangamivu ulio karibu.
15. Mali ya mtu tajiri ni mji wake wa nguvu;Uangamivu wa maskini ni umaskini wao.
16. Kazi yake mwenye haki huuelekea uzima;Mazao ya wabaya huuelekea dhambi.
17. Akubaliye kurudiwa huwa katika njia ya uzima;Bali yeye aachaye maonyo hukosa.