Mit. 10:7-14 Swahili Union Version (SUV)

7. Kuwakumbuka wenye haki huwa na baraka;Bali jina la mtu mwovu litaoza.

8. Aliye na akili moyoni mwake atapokea agizo;Bali mpumbavu mwenye maneno mengi ataanguka.

9. Aendaye kwa unyofu huenda salama;Bali apotoshaye njia zake atajulikana.

10. Akonyezaye kwa jicho huleta masikitiko;Bali mpumbavu mwenye maneno mengi ataanguka.

11. Kinywa chake mwenye haki ni chemchemi ya uzima;Bali jeuri hufunika kinywa chake mtu mwovu,

12. Kuchukiana huondokesha fitina;Bali kupendana husitiri makosa yote.

13. Hekima hupatikana midomoni mwa mwenye ufahamu;Bali fimbo hufaa kwa mgongo wake asiye na ufahamu.

14. Watu wenye akili huweka akiba ya maarifa;Bali kinywa cha mpumbavu ni uangamivu ulio karibu.

Mit. 10