27. Kumcha BWANA kwaongeza siku za mtu;Bali miaka yao wasio haki itapunguzwa.
28. Matumaini yao wenye haki yatakuwa furaha;Bali kutaraji kwao wasio haki kutapotea.
29. Njia ya BWANA ni kimbilio lake mtu mkamilifu;Bali ni uharibifu kwao watendao maovu.
30. Mwenye haki hataondolewa milele;Bali wasio haki hawatakaa katika nchi.
31. Kinywa cha mwenye haki hutoa hekima;Bali ulimi wa ukaidi utakatiliwa mbali.