Mit. 10:20-31 Swahili Union Version (SUV)

20. Ulimi wa mwenye haki ni kama fedha teule;Moyo wa mtu mbaya haufai kitu.

21. Midomo ya mwenye haki hulisha watu wengi;Bali wapumbavu hufa kwa kuwa hawana ufahamu.

22. Baraka ya BWANA hutajirisha,Wala hachanganyi huzuni nayo.

23. Kwa mpumbavu kutenda maovu ni kama mchezo;Bali mtu mwenye ufahamu ana hekima.

24. Aogopacho mtu asiye haki ndicho kitakachomjilia;Na wenye haki watapewa matakwa yao.

25. Kisulisuli kikiisha pita asiye haki hayuko tena;Bali mwenye haki ni msingi wa milele.

26. Kama siki menoni, na kama moshi machoni,Ndivyo alivyo mtu mvivu kwao wamtumao.

27. Kumcha BWANA kwaongeza siku za mtu;Bali miaka yao wasio haki itapunguzwa.

28. Matumaini yao wenye haki yatakuwa furaha;Bali kutaraji kwao wasio haki kutapotea.

29. Njia ya BWANA ni kimbilio lake mtu mkamilifu;Bali ni uharibifu kwao watendao maovu.

30. Mwenye haki hataondolewa milele;Bali wasio haki hawatakaa katika nchi.

31. Kinywa cha mwenye haki hutoa hekima;Bali ulimi wa ukaidi utakatiliwa mbali.

Mit. 10