2. Hazina za uovu hazifaidii kitu;Bali haki huokoa na mauti.
3. BWANA hataiacha nafsi ya mwenye haki ife na njaa;Bali tamaa ya mtu mwovu huisukumia mbali.
4. Atendaye mambo kwa mkono mlegevu huwa maskini;Bali mkono wake aliye na bidii hutajirisha.
5. Akusanyaye wakati wa hari ni mwana mwenye hekima;Bali asinziaye wakati wa mavuno ni mwana mwenye kuaibisha.
6. Baraka humkalia mwenye haki kichwani;Bali jeuri hufunika kinywa chake mtu mwovu.
7. Kuwakumbuka wenye haki huwa na baraka;Bali jina la mtu mwovu litaoza.
8. Aliye na akili moyoni mwake atapokea agizo;Bali mpumbavu mwenye maneno mengi ataanguka.
9. Aendaye kwa unyofu huenda salama;Bali apotoshaye njia zake atajulikana.