18. Yeye afichaye chuki ana midomo ya uongo,Na yeye asingiziaye ni mpumbavu.
19. Katika wingi wa maneno hapakosi kuwa na maovu;Bali yeye azuiaye midomo yake hufanya akili.
20. Ulimi wa mwenye haki ni kama fedha teule;Moyo wa mtu mbaya haufai kitu.
21. Midomo ya mwenye haki hulisha watu wengi;Bali wapumbavu hufa kwa kuwa hawana ufahamu.
22. Baraka ya BWANA hutajirisha,Wala hachanganyi huzuni nayo.
23. Kwa mpumbavu kutenda maovu ni kama mchezo;Bali mtu mwenye ufahamu ana hekima.
24. Aogopacho mtu asiye haki ndicho kitakachomjilia;Na wenye haki watapewa matakwa yao.