Mit. 10:18-24 Swahili Union Version (SUV)

18. Yeye afichaye chuki ana midomo ya uongo,Na yeye asingiziaye ni mpumbavu.

19. Katika wingi wa maneno hapakosi kuwa na maovu;Bali yeye azuiaye midomo yake hufanya akili.

20. Ulimi wa mwenye haki ni kama fedha teule;Moyo wa mtu mbaya haufai kitu.

21. Midomo ya mwenye haki hulisha watu wengi;Bali wapumbavu hufa kwa kuwa hawana ufahamu.

22. Baraka ya BWANA hutajirisha,Wala hachanganyi huzuni nayo.

23. Kwa mpumbavu kutenda maovu ni kama mchezo;Bali mtu mwenye ufahamu ana hekima.

24. Aogopacho mtu asiye haki ndicho kitakachomjilia;Na wenye haki watapewa matakwa yao.

Mit. 10