16. Kazi yake mwenye haki huuelekea uzima;Mazao ya wabaya huuelekea dhambi.
17. Akubaliye kurudiwa huwa katika njia ya uzima;Bali yeye aachaye maonyo hukosa.
18. Yeye afichaye chuki ana midomo ya uongo,Na yeye asingiziaye ni mpumbavu.
19. Katika wingi wa maneno hapakosi kuwa na maovu;Bali yeye azuiaye midomo yake hufanya akili.
20. Ulimi wa mwenye haki ni kama fedha teule;Moyo wa mtu mbaya haufai kitu.
21. Midomo ya mwenye haki hulisha watu wengi;Bali wapumbavu hufa kwa kuwa hawana ufahamu.
22. Baraka ya BWANA hutajirisha,Wala hachanganyi huzuni nayo.