Mit. 10:1-7 Swahili Union Version (SUV)

1. Mwana mwenye hekima humfurahisha babaye;Bali mwana mpumbavu ni mzigo wa mamaye.

2. Hazina za uovu hazifaidii kitu;Bali haki huokoa na mauti.

3. BWANA hataiacha nafsi ya mwenye haki ife na njaa;Bali tamaa ya mtu mwovu huisukumia mbali.

4. Atendaye mambo kwa mkono mlegevu huwa maskini;Bali mkono wake aliye na bidii hutajirisha.

5. Akusanyaye wakati wa hari ni mwana mwenye hekima;Bali asinziaye wakati wa mavuno ni mwana mwenye kuaibisha.

6. Baraka humkalia mwenye haki kichwani;Bali jeuri hufunika kinywa chake mtu mwovu.

7. Kuwakumbuka wenye haki huwa na baraka;Bali jina la mtu mwovu litaoza.

Mit. 10