1. Ole wao wakusudiao mambo maovu, na kutenda mabaya vitandani mwao! Kunapopambazuka asubuhi huyafanya, kwa sababu ya katika uwezo wa mikono yao.
2. Nao hutamani mashamba, na kuyashika; na nyumba pia, nao huzichukua; nao humwonea mtu na nyumba yake, naam, mtu na urithi wake.
3. Basi BWANA asema hivi, Angalia, nakusudia jambo baya juu ya jamaa hii, ambalo hamtazitoa shingo zenu, wala hamtakwenda kwa kiburi; kwa maana ni wakati mbaya.
4. Siku hiyo watatunga mithali juu yenu, na kuomboleza kwa maombolezo ya huzuni nyingi, na kusema,Sisi tumeangamizwa kabisa;Yeye analibadili fungu la watu wangu;Jinsi anavyoniondolea hilo!Awagawia waasi mashamba yetu.
5. Kwa hiyo hutakuwa na mtu atakayeitupa kamba kwa kura katika mkutano wa BWANA.
6. Msitabiri, ndivyo watabirivyo; wasiyatabiri mambo haya; lawama hazikomi.
7. Je! Litasemwa neno hili, enyi nyumba ya Yakobo, Roho ya BWANA imepunguzwa? Je! Haya ni matendo yake? Je! Maneno yangu hayamfai yeye aendaye kwa unyofu?