Mhu. 8:1-13 Swahili Union Version (SUV)

1. Ni nani aliye kama mwenye hekima;Naye ni nani ajuaye kufasiri neno?Hekima ya mtu humng’ariza uso wake,Na ugumu wa uso wake hubadilika.

2. Mimi nasema hivi, Uishike amri ya mfalme; na hiyo kwa sababu umeapa kwa Mungu.

3. Usifanye haraka kutoka mbele ya uso wake; usiendelee kufanya lililo baya; maana yeye hufanya lo lote limpendezalo.

4. Kwa kuwa neno la mfalme lina nguvu; naye ni nani awezaye kumwambia huyo, Wafanya nini?

5. Aishikaye amri hatajua neno baya;Na moyo wa mwenye hekima hujua wakati na hukumu.

6. Kwa maana kwa kila shauri kuna wakati na hukumu; kwa sababu mashaka ya mwanadamu yaliyo juu yake ni makubwa;

7. kwa kuwa hajui yatakayokuwako; kwa maana ni nani awezaye kumweleza jinsi yatakavyokuwa?

8. Hakuna mwenye uwezo juu ya roho aizuie roho;Wala hana mamlaka juu ya siku ya kufa;Wala hakuna kuruhusiwa katika vita vile;Wala uovu hautamwokoa yule aliyeuzoea.

9. Mambo hayo yote nimeyaona, nikatia moyo wangu katika kila kazi iliyofanyika chini ya jua. Kuna wakati ambapo mtu mmoja anayo mamlaka juu ya mwenziwe kwa hasira yake.

10. Pia nikaona waovu wamezikwa, nao wamefika kaburini; tena waliofanya mema wameondoka katika patakatifu, nao wamesahauliwa mjini. Hayo nayo ni ubatili.

11. Kwa sababu hukumu juu ya tendo baya haitekelezwi upesi, mioyo ya wanadamu huthibitishwa ndani yao ili kutenda mabaya.

12. Ajapokuwa mwenye dhambi amefanya maovu mara mia, akazidisha siku zake; lakini hata hivyo najua hakika ya kwamba itakuwa heri kwao wamchao Mungu, wenye kicho mbele zake;

13. walakini haitakuwa heri kwa mwovu, wala hatazidisha siku zake, zilizo kama kivuli; kwa sababu hana kicho mbele za Mungu.

Mhu. 8