1. Mkumbuke Muumba wako siku za ujana wako,Kabla hazijaja siku zilizo mbaya,Wala haijakaribia miaka utakaposema,Mimi sina furaha katika hiyo.
2. Kabla jua, na nuru, na mwezi,Na nyota, havijatiwa giza;Kabla ya kurudi mawingu baada ya mvua;
3. Siku ile walinzi wa nyumba watakapotetema;Hapo wenye nguvu watakapojiinamisha;Na wasagao kukoma kwa kuwa ni haba;Na hao wachunguliao madirishani kutiwa giza;
4. Na milango kufungwa katika njia kuu;Sauti ya kinu itakapokuwa ni ndogo;Na mtu kusituka kwa sauti ya ndege;Nao binti za kuimba watapunguzwa;