Mhu. 12:1-4 Swahili Union Version (SUV)

1. Mkumbuke Muumba wako siku za ujana wako,Kabla hazijaja siku zilizo mbaya,Wala haijakaribia miaka utakaposema,Mimi sina furaha katika hiyo.

2. Kabla jua, na nuru, na mwezi,Na nyota, havijatiwa giza;Kabla ya kurudi mawingu baada ya mvua;

3. Siku ile walinzi wa nyumba watakapotetema;Hapo wenye nguvu watakapojiinamisha;Na wasagao kukoma kwa kuwa ni haba;Na hao wachunguliao madirishani kutiwa giza;

4. Na milango kufungwa katika njia kuu;Sauti ya kinu itakapokuwa ni ndogo;Na mtu kusituka kwa sauti ya ndege;Nao binti za kuimba watapunguzwa;

Mhu. 12