21. Wakamwuliza, wakisema, Mwalimu, twajua ya kwamba wasema na kufundisha yaliyo ya haki, wala hujali cheo cha mtu, bali unafundisha njia ya Mungu kwa kweli.
22. Je! Ni halali tumpe Kaisari kodi, au sivyo?
23. Lakini yeye alitambua hila yao, akawaambia,
24. Nionyesheni dinari. Ina sura na anwani ya nani? Wakamjibu, Ya Kaisari.
25. Akawaambia, Basi, vya Kaisari mpeni Kaisari, na vya Mungu mpeni Mungu.
26. Wala hawakuweza kumshitaki kwa maneno yake mbele ya watu; wakastaajabia majibu yake, wakanyamaa.
27. Kisha baadhi ya Masadukayo wakamwendea, wale wasemao ya kwamba hakuna ufufuo, wakamwuliza,
28. wakisema, Mwalimu, Musa alituandikia ya kuwa, mtu akifiwa na ndugu yake mwenye mke, lakini hana mtoto na amtwae huyu mke, ampatie ndugu yake mzao.
29. Basi, kulikuwa na ndugu saba. Wa kwanza alioa mke, akafa hana mtoto;
30. na wa pili [akamtwaa yule mke, akafa hana mtoto;]
31. hata wa tatu akamwoa, na kadhalika wote saba, wakafa, wasiache watoto.
32. Mwisho akafa yule mke naye.