20. Wazijua amri; Usizini, Usiue, Usiibe, Usishuhudie uongo, Waheshimu baba yako na mama yako.
21. Akasema, Hayo yote nimeyashika tangu utoto wangu.
22. Yesu aliposikia hayo alimwambia, Umepungukiwa na neno moja bado; viuze ulivyo navyo vyote, ukawagawanyie maskini, nawe utakuwa na hazina mbinguni; kisha, njoo unifuate.
23. Lakini aliposikia hayo alihuzunika sana, maana alikuwa na mali nyingi.