11. Ikawa walipokuwa njiani kwenda Yerusalemu, alikuwa akipita katikati ya Samaria na Galilaya.
12. Na alipoingia katika kijiji kimoja, alikutana na watu kumi wenye ukoma; wakasimama mbali,
13. wakapaza sauti wakisema, Ee Yesu, Bwana mkubwa, uturehemu!
14. Alipowaona aliwaambia, Enendeni, mkajionyeshe kwa makuhani. Ikawa walipokuwa wakienda walitakasika.
15. Na mmoja wao alipoona kwamba amepona, alirudi, huku akimtukuza Mungu kwa sauti kuu;
16. akaanguka kifudifudi miguuni pake, akamshukuru; naye alikuwa Msamaria.
17. Yesu akajibu, akanena, Hawakutakaswa wote kumi? Wale kenda wa wapi?
18. Je! Hawakuonekana waliorudi kumpa Mungu utukufu ila mgeni huyu?
19. Akamwambia, Inuka, enenda zako, imani yako imekuokoa.
20. Na alipoulizwa na Mafarisayo, Ufalme wa Mungu utakuja lini? Aliwajibu akawaambia, ufalme wa Mungu hauji kwa kuuchunguza;
21. wala hawatasema, Tazama, upo huku, au, kule, kwa maana, tazama, ufalme wa Mungu umo ndani yenu.
22. Akawaambia wanafunzi, Siku zitakuja mtakapotamani kuona siku moja katika siku zake Mwana wa Adamu, msiione.
23. Tena watawaambia, Tazama, kule! Tazama, huku! Msiondoke mahali mlipo, wala msiwafuate;