Lk. 13:6-12 Swahili Union Version (SUV)

6. Akanena mfano huu; Mtu mmoja alikuwa na mtini umepandwa katika shamba lake la mizabibu; akaenda akitafuta matunda juu yake, asipate.

7. Akamwambia mtunzaji wa shamba la mizabibu, Tazama, miaka mitatu hii naja nikitafuta matunda juu ya mtini huu, nisipate kitu; uukate, mbona hata nchi unaiharibu?

8. Akajibu akamwambia, Bwana, uuache mwaka huu nao, hata niupalilie, niutilie samadi;

9. nao ukizaa matunda baadaye, vema! La, usipozaa, ndipo uukate.

10. Siku ya sabato alikuwa akifundisha katika sinagogi mojawapo.

11. Na tazama, palikuwa na mwanamke aliyekuwa na pepo wa udhaifu muda wa miaka kumi na minane, naye amepindana, hawezi kujinyosha kabisa.

12. Yesu alipomwona alimwita, akamwambia, Mama, umefunguliwa katika udhaifu wako.

Lk. 13