Lk. 12:57-59 Swahili Union Version (SUV)

57. Na mbona ninyi wenyewe kwa nafsi zenu hamwamui yaliyo haki?

58. Maana, unapofuatana na mshitaki wako kwenda kwa mwamuzi, hapo njiani fanya bidii kupatanishwa naye, asije akakuburuta mpaka mbele ya kadhi; yule kadhi akakutia mikononi mwake mwenye kulipiza, na yule mwenye kulipiza akakutupa gerezani.

59. Nakuambia, Hutoki humo kamwe hata uishe kulipa senti ya mwisho.

Lk. 12