57. Na mbona ninyi wenyewe kwa nafsi zenu hamwamui yaliyo haki?
58. Maana, unapofuatana na mshitaki wako kwenda kwa mwamuzi, hapo njiani fanya bidii kupatanishwa naye, asije akakuburuta mpaka mbele ya kadhi; yule kadhi akakutia mikononi mwake mwenye kulipiza, na yule mwenye kulipiza akakutupa gerezani.
59. Nakuambia, Hutoki humo kamwe hata uishe kulipa senti ya mwisho.