Lk. 12:29-33 Swahili Union Version (SUV)

29. Ninyi msitafute mtakavyokula wala mtakavyokunywa; wala msifanye wasiwasi,

30. kwa maana, hayo yote ndiyo watafutayo mataifa ya duniani, lakini Baba yenu anajua ya kuwa mna haja na hayo.

31. Bali utafuteni ufalme wa Mungu, na hayo mtaongezewa.

32. Msiogope, enyi kundi dogo; kwa kuwa Baba yenu ameona vema kuwapa ule ufalme.

33. Viuzeni mlivyo navyo, mtoe sadaka. Jifanyieni mifuko isiyochakaa, akiba isiyopungua katika mbingu, mahali pasipokaribia mwivi, wala nondo haharibu.

Lk. 12