Kut. 40:13-17 Swahili Union Version (SUV)

13. Kisha utamvika Haruni mavazi matakatifu; nawe utamtia mafuta, na kumweka awe mtakatifu, ili apate kunitumikia katika kazi ya ukuhani.

14. Kisha utawaleta wanawe, na kuwavika kanzu zao;

15. nawe utawatia mafuta kama ulivyomtia mafuta baba yao, ili wanitumikie katika kazi ya ukuhani; na huko kutiwa mafuta kwao kutakuwa ni kwa ukuhani wa milele katika vizazi vyao vyote.

16. Musa akafanya hayo yote; kama yote BWANA aliyoagiza ndivyo alivyofanya.

17. Hata mwezi wa kwanza wa mwaka wa pili, siku ya kwanza ya mwezi ile maskani ilisimamishwa.

Kut. 40