Kut. 36:20-32 Swahili Union Version (SUV)

20. Kisha akafanya mbao za mti wa mshita kwa hiyo maskani, zilizosimama.

21. Urefu wa kila ubao ulikuwa ni dhiraa kumi, na upana wa kila ubao ulikuwa ni dhiraa moja na nusu.

22. Kila ubao ulikuwa na ndimi mbili, zilizounganywa pamoja; ndivyo alivyozifanya hizo mbao zote za maskani.

23. Naye akazifanya hizo mbao kwa ajili ya hiyo maskani; mbao ishirini kwa upande wa kusini kuelekea kusini;

24. naye akafanya matako ya fedha arobaini yawe chini ya hizo mbao ishirini; matako mawili chini ya ubao mmoja kwa hizo ndimi zake mbili, na matako mawili chini ya ubao mwingine kwa ndimi zake mbili.

25. Na kwa upande wa pili wa maskani upande wa kaskazini, akafanya mbao ishirini,

26. na matako yake ya fedha arobaini; matako mawili chini ya ubao mmoja, na matako mawili chini ya ubao mwingine.

27. Na kwa upande wa nyuma wa hiyo maskani kuelekea magharibi akafanya mbao sita.

28. Naye akafanya mbao mbili kwa pembe za maskani upande wa nyuma.

29. Nazo zilikuwa mbao pacha upande wa chini, vivyo zilishikamana pamoja hata ncha ya juu kufikilia pete ya kwanza; ndivyo alivyofanya zote mbili katika hizo pembe mbili.

30. Hivyo zilikuwa mbao nane, na matako yake ya fedha, matako kumi na sita, matako mawili chini ya kila ubao.

31. Kisha akafanya mataruma ya miti ya mshita; matano kwa mbao za upande mmoja wa maskani;

32. na mataruma matano kwa mbao za upande wa pili wa maskani, na mataruma matano kwa hizo mbao za maskani zilizokuwa upande wa nyuma kuelekea magharibi.

Kut. 36