Kut. 29:9-11 Swahili Union Version (SUV)

9. Nawe uwakaze mishipi, Haruni na wanawe, na kuwavika kofia; nao watakuwa na huo ukuhani kwa amri ya milele; nawe utawaweka Haruni na wanawe kwa kazi takatifu.

10. Kisha utamleta huyo ng’ombe mbele ya hema ya kukutania; na Haruni na wanawe wataweka mikono yao juu ya kichwa cha huyo ng’ombe.

11. Kisha utamchinja huyo ng’ombe mbele ya BWANA, mlangoni pa hema ya kukutania.

Kut. 29