Kut. 15:12-23 Swahili Union Version (SUV)

12. Ulinyosha mkono wako wa kuume,Nchi ikawameza.

13. Wewe kwa rehema zako umewaongoza watu uliowakomboa,Kwa uweza wako uliwaelekeza hata makao yako matakatifu.

14. Kabila za watu wamesikia, wanatetemeka,Wakaao Ufilisti utungu umewashika.

15. Ndipo majumbe wa Edomu wakashangaa,Watu wa Moabu wenye nguvu tetemeko limewapata,Watu wote wakaao Kanaani wameyeyuka.

16. Hofu na woga umewaangukia;Kwa uweza wa mkono wako wanakaa kimya kama jiwe;Hata watakapovuka watu wako, Ee BWANA,Hata watakapovuka watu wako uliowanunua.

17. Utawaingiza, na kuwapanda katika mlima wa urithi wako,Mahali pale ulipojifanyia, Ee BWANA, ili upakae,Pale patakatifu ulipopaweka imara, BWANA, kwa mikono yako.

18. BWANA atatawala milele na milele.

19. Kwa maana farasi za Farao na magari yake na wapanda farasi wake waliingia ndani ya bahari, BWANA akayarudisha maji ya bahari juu yao; bali wana wa Israeli walikwenda katika nchi kavu katikati ya bahari.

20. Na Miriamu, nabii mke, ndugu yake Haruni, akatwaa tari mkononi mwake; wanawake wakatoka wote wakaenda nyuma yake, wenye matari na kucheza.

21. Miriamu akawaitikia,Mwimbieni BWANA kwa maana ametukuka sana;Farasi na mpanda farasi amewatupa baharini.

22. Musa akawaongoza Israeli waende mbele kutoka Bahari ya Shamu, nao wakatokea kwa jangwa la Shuri; wakaenda safari ya siku tatu jangwani wasione maji.

23. Walipofika mahali palipoitwa Mara hawakupata kuyanywa yale maji ya Mara, kwa kuwa yalikuwa machungu; kwa ajili ya hayo jina lake likaitwa Mara.

Kut. 15