1. Ndipo Musa na wana wa Israeli wakamwimbia BWANA wimbo huu wakanena, na kusema,Nitamwimbia BWANA, kwa maana ametukuka sana;Farasi na mpanda farasi amewatupa baharini.
2. BWANA ni nguvu zangu, na wimbo wangu;Naye amekuwa wokovu wangu.Yeye ni Mungu wangu, nami nitamsifu;Ni Mungu wa baba yangu, nami nitamtukuza.